Harmonize
Matatizo
"Matatizo" - Harmonize
[Intro]
Haiyee Aaah!!
Wasafi records
Olelelelee

[Verse 1]
Alfajiri imefika
Anga inang'aa
Mvua inaanza katika
Ghafla tumbo la njaa
Naweka sauti kwa spika
Nipate umbea wa Dar
Mara simu inaita
Jina la Uncle Twaha
Akisema, mama yu hoi kitandani
Kama si wa leo wa kesho
Na kupona sizani
Upate japo neno la mwisho
Mi ndo mtoto wa pekee
Nyumbani wananitegemea
Mdogo wangu wa kike
Hali duni alishaga olewa
Tizama jasho langu la mnyonge
Kipato hakikidhi mahitaji
Napiga moyo konde
Yarabi mola ndo mpaji
[Chorus]
Matatizo Matatizo
Yatakwisha lini
Matatizo
Kila siku mimi
Ewe mola
Matatizo yatakwisha lini
Japo likizo
Nifurahi na mimi

[Verse 2]
Mola aliniumba na subira
Imani pekee ngao yangu
Mbona nishasali sana
Ila mambo bado tafalani
Mama kanifunza kikabila
Nikonde sana haini yangu
Tena nijitume sana
Na vya watu nisivitamani
Hata mpenzi niliyenae
Najua siku atanikimbia
Itanitesa ye ndo nguzo
Zile ngoja kesho badae
Atazichoka kuzivumilia
Anakosa hata matunzo
[Bridge]
Ona, nadaiwa kodi nilipopanga
Nashinda road nikihanda
Nishapiga hodi kwa waganga
Kwa kuhisi narogwa
Nikauza maji na karanga
Nikawa dobi kwa viwanda
Ila kote ziro ni majanga
Mtindo mmoja

[Pre Chorus]
Mi ndo mtoto wa pekee
Nyumbani wananitegemea
Mdogo wangu wa kike
Hali duni alishagaolewa
Tizama jasho langu la mnyonge
Kipato hakikidhi mahitaji
Napiga moyo konde
Yarabi mola ndo mpaji

[Chorus]
Matatizo. matatizo
Yatakwisha lini
Ewe Mola
Matatizo
Kila siku mimi
Jamani Matatizo
Matatizo Ooh matatizo
Yatakwisha lini
Japo likizo
Nifurahi na mimi
Matatizo. matatizo
Yatakwisha lini
Matatizo
Kila siku mimi
Jamani Matatizo
Matatizo matatizo
Yatakwisha lini
Japo likizo
Nifurahi na mimi