Bonobo
NIKO HOME
VERSE 1:BONOBO
Kila rapa mkali nyuma kuna ghost writer
Wabana pua nyuma kuna boss taita
Je unataka bifu?,ok niko na punch moto lighter
Mfano wa masihi jinsi nitavyopaa kwa hyo cypher
Niko na line na sihitaji sign ya marapa
Nimeshine utuli fine by falsafa
Veteran break defence kama ngasa
Shout kwa makanta na kinasa nipo hapa sasa
Nilipowaza kuwa jana masta
Hakuna kichwa kitachompima papa wa nyasa
Huyu bonobo ndio wa wapi?mbona mi sijui
Ila ninavyopita kwenye mdundo kuna kitu ugundui
Vipi wanafunzi kama we mwalimu utambui
Frontline na mabango ya upendo moyo umejaa uadui
Mnakunja hamkunjui mnatubana hatupumui
Tunatoboa mbele yenu kwa sababu hamsumbui

Hook:BONOBO
Shout kwa mr two sugu nipo home nipo home
Isanga family uswahilini matola yeah niko home
Wasadikaya makanta niko home niko home
Shout to everybody mbeya city babebeibe

VERSE 2: BONOBO
Niko home mitaa ya kabwe
Ukija kibishoo lazima ukabwe
Chocho kibao na michongo inayofanyika ya mazabe
Tunaishi na watu wazito zaidi ya kabwe
Na pesa inatafutwa kama tumepotеza
Na haina kususa kusua sua kwenye fedha
Wahuni wananusa chunga sana usijе teleza
Rip MBUZA harakati naendeleza
Nawakoma kumwanya tena sana
Na run uyole mpaka ghana toka zama
Wana wana alosto hii voko ya gharama
Na kila nikiflow tunapaa si ni ndege tunaofanana
BLOCK T,AIRPORT,MBALIZI
Nikitaka balizi fukwe matema beach
TUKUYU ndizi na maparachichi
Huu ni zaidi ya urith mbeya yetu sisi
Hook:BONOBO
Shout to nonde mpaka ghana niko home niko
Kabwe mpaka sido niko home niko home
Sai mama john na mbalizi niko home niko home
Ilolo makunguru mabatini simike niko home niko home

Outro;
Naomba kutumia nafasi kama hii kujitambulisha kwenu
Naitwa freshking aka bonobo aka papa wa nyasa
Niko home round hii,im from mbeya city aka hip hop city
Im from mbeya city aka green city